Na Fatma Gaffus,
Dodoma.
Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa mkoani Dodomaimenunua madawati 525 yenye thamani ya shilingi milioni 36.5 na kuyasambaza katika shule 53 za Msingi wilayani humo.
Akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bwana Athman Akalama alisema lengo ni kupunguza tatizo la wanafunzi kukaa chini.
Afisa Elimu ya Msingi wa Wilaya ya Kongwa Bwana Ligola Michael alisema kati ya wanafunzi 55,848, wanaokaa kwenye madawati ni 29,841 na wengine 26,007 wanakaa chini.
Aidha alisema kiasi cha shilingi milioni 40 kimetumika kwa ajili ya ujenzi wa Maabara katika shule ya sekondari Zoissa.
Wilaya ya Kongwa ina shule za msingi 105 zenye wanafunzi 55,848.
Mahitaji ya madawati ni 18,616 na yaliyopo ni madawati 9,947 na upungufu ni madawati 8,669.
Mwisho.











NAOMBA WILAYA YA KONGWA ICHUNGUZWE KWANI WAFANYAKAZI WENGI HAWANA SIFA HASA IDARA YA ELIMU KWAN WANASHINDWA KUWAJIBIKA ILA WANAWEZA KUKATA MISHAHARA YA WALIMU NDO FANI YAO.KWAN MATATIZO YA WALIMU NI MAKUBWA SANA.LAKINI HATA HAWASIKILIZI .JIBU FUATILIA MATOKEO YA MWAKA KATIKA WILAYA YA KONGWA NI UOZO MTUPU.NABADO KUGOMA SIO KUKAA BARABRANI///
SIO HIVYO TU WALIMU WENGI WAMEPANDISHWA MADARAJA MIAKA ZAIDI YA SABA MPAKA LEO HAWAJABADILISHIWA MISHAHARA YAO KWANINI? JIBU NI UFISADI ULIOKITHIRI KATIKA WILAYA YA KONGWA,LAKIN WAHUSIKA WAPO WANAUZA SURA NA KUPAKA PODA MAOFISINI.TUTAFIKA KWA PHILOSOPHY YA ARI YA ZAMANI,NGUVU YA ZAMAN,NA TUNASONGA NYUMA
MABOSI TUME YA UTUMISHI NI MAJINA TU KWANI HAWANA LOLOTE,MATOKEO YA SHULE ZA KATA MAARUFU KAMA KAYUMBA SEC SCHOOL YA KIDATO CHA NNE NI UOZO MTUPU NA BADO WATAFELI MPAKA WAKOME.SISI KAMA WALIMU TUTAENDELEZA KUFELISHA HADI PALE TUTAKAPOSIKILIZWA MATATIZO YETU.