Na Kasilda Mlimila, Morogoro
Wakati huo huo, mgomo wa madaktari ulioanza Januari 24 mwaka huu katika hospitali ya taifa Muhimbili na kusambaa kwenye mikoa ya Dodomana Mbeya sasa umetua mkoani Morogoro baada ya madaktari wa hospitali kuu ya Mkoa kugoma na kusababisha tahaluki kubwa kwa wagonjwa.
Mgomo huo wa madaktari katika hospitali ya Mkoa umeanza mapema asubuhi ya Januari 26 ambapo kwa mujibu wa wagonjwa waliozungumza na Star Tv hospitalini hapo hakuna hata mgonjwa mmoja aliyepatiwa matibabu.
Wagonjwa hao wameiomba serikali kushughulikia madai ya madaktari ili waweze kusitisha mgomo na hivyo kuokoa maisha ya wagonjwa wengi waliopo hospitalini hapo ambao hali zao ni mbaya kutokana na kukosa matibabu.
Hata hivyo Star Tv ilipotaka kupata maelezo kutoka kwa uongozi hospitalini hapo kuhusiana na mgomo huo imeelezwa kuwa Mganga Mkuu wa Mkoa yupo safarini kikazi na viongozi wengine waliobakia katika hospitali hawakuwa tayari kuzungumzia lolote kuhusiana na mgomo huo.
Star Tv ilipowafuata madaktari waliokuwa katika mkutano kwenye moja ya majengo yaliyopo hospitalini hapo ili wazungumzie mgomo wao wamekataa katakata kuongea ama kupigwa picha.
Mwisho











SERIKARI INATAKIWA KUJALI MAHITAJI YA MADAKTARI KUPUNGUZA MAAFA YA VIFO.