Wednesday February 22nd 2012

Pinda: Serikali ipo katika mikakati ya uboreshaji kilimo.

Na Joseph Mpangala,                          

Dar es Salaam. 

Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda amesema Serikali ipo katika mikakati ya kuhakikisha sekta ya kilimo inaboreshwa kwa kuwawezesha wakulima kuzalisha chakula cha ziada watakachokiuza na kujiongezea kipato.

Waziri Mkuu Pinda amebainisha mikakati hiyo kwenye mkutano wa siku mbili baina ya Wizara ya Fedha na Wadau wa Maendeleo unaojadili masuala ya Maendeleo na Uchumi.

Ingawa sekta ya kilimo inachukua asilimia 80 ya wananchi wote waTanzaniakwa kujishughulisha na kilimo cha mazao ya chakula na biashara lakini bado sekta hiyo haijapewa kipaumbele cha kutosha ili kumwezesha kila mwananchi anayejishughulisha na kilimo anufaike kikamilifu.

Akiongea mara baada ya kufungua mkutano wa siku mbili wa wadau wa maendeleo, Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda amesema ili kuhakikisha sekta ya kilimo inafanya vizuri ni lazima taasisi zisizo za kiserikali pamoja na Sekta binafsi kuhakikisha zinashiriki kikamilifu kwa kutoa mawazo na msaada wa kifedha kwa wakulima nchini.

Nao wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo wanaoshiriki mkutano huo wamesema bila kutafuta soko la uhakika kwa wakulima wadogo pamoja uboreshaji wa miundombinu na nishati ya umeme kwa ajili ya kuhifadhia mazaoyaobado juhudi za kuwanua kiuchumi wakulima nchini zitaendelkea kukabiliwa na changamoto kubwa.

Hata hivyo wajibu wa Serikali unaonesha kuwa uboreshaji wa masoko ya mazao ya kilimo na biashara pamoja na uuzaji wa mazao kwa kutumia sayansi na teknolojia unatakiwa kuimarishwa kwa kuwaelimisha kabla ya kuuza bidhaa zao.

 

Mwisho

Leave a Comment

More from category

Zaidi ya magari 200 yakwama mpakani Holili
Zaidi ya magari 200 yakwama mpakani Holili

Na Enos Masanja, Moshi.  Zaidi ya magari 200 yanayosafirisha mzigo kupitia mpaka wa Holili juzi yamekwama kwa zaidi ya [Read More]

Zana za uchimbaji,  Wachimbaji Wadogo kunufaika kanda ya kati.
Zana za uchimbaji, Wachimbaji Wadogo kunufaika kanda ya kati.

Na Emmanuel Michael, Singida.  Wachimbaji wadogo wa madini ya aina mbalimbali kanda ya kati wanatarajiwa kuondokana na [Read More]

Umeme wa jua, Wakazi Kiagata Musoma kuanza kunufaika.
Umeme wa jua, Wakazi Kiagata Musoma kuanza kunufaika.

Na Mabere Makubi,             Musoma.  Wakazi wa vijiji 14 vya Tarafa ya Kiagata Wilaya ya Musoma vijijini [Read More]

Uwepo mgao wa umeme, Waziri wa Nishati na Madini akanusha.
Uwepo mgao wa umeme, Waziri wa Nishati na Madini akanusha.

Na Ivona Kamuntu, Mwanza.  Waziri wa Nishati na Madini Mheshimiwa William Ngeleja amekanusha kuwa hakuna mgao wa umeme [Read More]

Sekta ya Utalii Mwanza,  Miundombinu na uwanja wa ndege vikwazo
Sekta ya Utalii Mwanza, Miundombinu na uwanja wa ndege vikwazo

Na Rogers William,Mwanza.  Tatizo la miundombinu na ukosefu wa uwanja wa ndege wa kisasa katika jiji la Mwanza [Read More]