Wednesday February 22nd 2012

Usafiri reli ya kati waanzia Dodoma.

Na Fatma Gaffus, Dodoma. 

Usafiri wa Reli ya Kati umeanza wakati ujenzi katika Daraja la Godegode wilayani Mpwapwa ukiendelea.

Akizungumza na Star Tv, Mkuu wa Kituo wa Kampuni ya Reli Mkoa wa Dodoma Bwana Flavian Nyawale amesema wamechukua hatua hiyo ya kuanza huduma za safari za Treni kutokaDodomakwenda Kigoma kutokana na maeneo ya Gulwe, Godegode na Kidete kuwa korofi kwa sababu ya mvua kubwa zinazoendelea kunyesha mkoaniDodoma.

Bwana Nyawale amesema kuhusu Treni ya kwenda Mwanza bado haijaanza safari zake kwa sababu wanatafuta fedha za kuweza kutoa huduma hiyo.

Amesema huduma ya usafiri itakuwa inatolewa mara mbili kwa wiki kwa siku ya Jumanne na Jumamosi ambapo Treni za mizigo zinaendelea kupita katika daraja la Godegode wakati ujenzi ukiendelea kwa uangalizi mkubwa.

Baadhi ya Abiria waliosafiri na Treni hiyo ya abira iliyoondoka Januari 24 majira ya saa 1.15 usiku wameishukuru Kampuni ya Reli TRL kwa kuanza kuwapatia huduma hiyo muhimu ambayo waliikosa kwa muda mrefu sasa.

Wamesema walisitisha safari zao kwa kushindwa kumudu gharama za mabasi hasa katika kipindi cha kumaliza likizo kwa wafanyakazi na wanafunzi.

Wameitaka Kampuni ya Reli TRL kushughulikia kero zote ambazo zinajitokeza katika zoezi zima la kurudisha fedha kwa abiria pindi itakapotokea tena hali hiyo ya kukosa huduma za usafiri katika msimu wa mvua ambapo maeneo ya Gulwe, Godegode na Kidete yanakuwa yakisumbua kipindi hicho.  

Takribani siku 36 huduma za usafiri katika Kampuni hiyo ilisitisha huduma zake kutokana na kuharibika kwa daraja la Godegode hali iliyosababisha Kampuni hiyo kuwasafirisha abiria wake kwa njia ya barabra kwa kutumia mabasi kutokaDodomakwenda Dar es Salaam.

 

Mwisho.

 

 

Leave a Comment

More from category

Mgogoro CUF, Wananchi waendelea kujivua uanachama
Mgogoro CUF, Wananchi waendelea kujivua uanachama

Na Beatrice Ojjiki, Dar es Salaam.                               Chama cha wananchi CUF [Read More]

Wananchi walalamikia viongozi Gairo.
Wananchi walalamikia viongozi Gairo.

Na Kasilda Mlimila, Morogoro. Wananchi wa Gairo wilayani Kilosa, mkoa wa Morogoro wanakabiliwa na kero mbalimbali [Read More]

Ajali ya moto, Kiwanda cha samani za ndani chateketea Dar.
Ajali ya moto, Kiwanda cha samani za ndani chateketea Dar.

Na Faraji Mwagowa, Dar Es Salaam. MOTO mkubwa umezuka na kuteketeza kiwanda cha samani za ndani na baadhi ya maduka [Read More]

Chakula cha ziada, Hatua za dharura za muda mrefu zahitajika
Chakula cha ziada, Hatua za dharura za muda mrefu zahitajika

Na Joseph Mpangala,                                     Dar es Salaam. Mkutano wa [Read More]

Maeneo ya kimila ya kimasai, Ukuaji mji wa Monduli hatarini kuyapoteza.
Maeneo ya kimila ya kimasai, Ukuaji mji wa Monduli hatarini kuyapoteza.

Na Ramadhan Mvungi, Arusha.  Kasi ya kupanuka kwa Mji wa Monduli mkoani Arusha imetishia kutoweka kwa maeneo ya [Read More]