Copyright @ STAR TV LTD . All Rights Reserved.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam,Mkurugenzi Mtendaji wa Bank ya Exim Bi Sabetha Mwambenja amesema sekta ya fedha hapa nchini itakuwa endapo jamii itashirikishwa katika masuala ya mzunguko wa fedha ukiwepo wa ukopeshaji.
Kwa kiasi gani benki yake imeweza kuisaidia jamii bibi Bi Sabetha amesema wameongeza mikopo kutoka shilingi bilioni 205 hadi 264 kuanzia mwaka 2008 hadi mwaka huu wa 2010 .
Sambamba na kuisaidia jamii benki ya Exim inampango kufungua matawi zaidi kwenye mikoa ya Manyara , Iringa pamoja na nchi za Djibout na Zambia .
Ameyataja baadhi ya masharti ambayo Banki kuu ya Tanzania kwa ajili ya kufungua matawi nje ya nchi kuwa na mtaji wa zaidi ya bilioni 50 pamoja na kuyaunganisha matawi ya nchi hizo na makao makuu ya benki hiyo.
Bongo Beats every Monday to Saturday @ 1900hrs
Bonga na Startv every Monday to Saturday @ 1705hrs
Habari every Monday to Sunday @ 2000hrs