Amesema sherehe za kuwasha mwenge wa uhuru zitafanyika katika kijiji cha Msoga Wilayani Bagamoyo eneo ambalo ndiko alikozaliwa Rais Jakaya Kikwete na kwamba mgeni rasmi atakuwa ni Waziri mkuu Mizengo Pinda.
Amesema mbio hizo mwenge wa uhuru zintarajiwa kupitia katika miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye sekta ya Elimu, Afya, mazingira na kilimo.
Dkt Ishengoma amesema miongoni mwa maandalizi yanayoendelea vema ni pamoja na mazoezi ya kuwasha mwenge huo ambayo yanafanywa na wanafunzi 600 kutoka katika shule mbalimbali za msingi zilizopo katika kijiji hicho cha Msoga,usafi na ukataji nyasi kwa ajili ya ujenzi wa eneo la kiwanja kitakachotumika katika shughuli nzima ya kuwasha mwenge huo.
Amesema pamoja na maandalizi hayo kuendelea vema bado mkoa huo unahitaji wahisani wengine wajitokeze kuchangia fedha na hata magari kwa ajli ya kusaidia katika shughuli nyingine za kukimbiza mwenge huo wa Uhuru ingawa tayari wapo wafadhili ambao wamejitokeza kuchangia michango yao lakini bado haijatosheleza mahitaji.
Mkuu huyo wa mkoa amewataka wakuu wa wilaya zote kuhakikisha miradi yote iliyopangwa kupitiwa na kuzinduliwa katika mbio hizo za mwenge wa uhuru imekamilika na pia amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye sherehe hiyo ua kuzindua mbio za mwenge huo mwaka huu.
Hii ni mara ya kwanza kwa mkoa wa Pwani kuwasha mbio za mwenge hivyo mwaka huu itakuwa ni historia kubwa kwa wakazi mkoani humu.
Desemba 18 mwaka jana Serikali ilipiga marufuku utaratibu wa njia za Mwenge wa uhuru kujirudia kwenye maeneo yaliyowahi kupita katika Wilaya zote nchini wakati kuna sehemu nyingine ambazo hazijapata bahati ya kupitiwa na matembezi hayo tangu nchi ipate uhuru .
Hatua hiyo ya Seikali kupiga maarufuku urudiaji wa njia za Mwenge wa uhuru imekuja baada ya kuwepo kwa Wilaya nyingi nchini ambazo zimekuwa zikipitisha matembezi hayo kwa kurudia maeneo kwa kisingizio cha ubovu wa miundo mbinu na hivyo kuwakosesha wananchi haki ya kuuona mwenge.
Tamko hilo lilitolewa na aliyekuwa Waziri wa Kazi,ajira na maendeleo ya vijana John Chiligari ambaye alisema tathinimi imeonyesha kuwa katika wilaya nyingi kila mwaka njia za mwenge wa Uhuru hujirudia wakati kuna maeneo mengine tangu nchi ipate uhuru wananchi wake hawaja wahi kuuona hivyo mwakani lazima kufanyike mabadiliko mbio za mwenge zipite kwenye maeneo ambayo hayajawahi kupitiwa na mbio hizo.
Chiligati alisema wanachi katika maeneo hayo wana haamu kubwa ya kuuona mwenge wao wa uhuru lakini wamekuwa wakiusikia tu kupitia vyomba vya habari hivyo kusababisha hata kusahaulika katika masuala mbalimbali ya maendeleo kama ile ya miundo mbinu kwani maeneo mengi yaliyopitishwa mbia hizo zimekuwa zikinufaika kwa kuchongwa barabara na hata miradi mingineyo kupata bahati ya kuibuliwa.
Aliongeza kwa kuitaka Mkoa utakaozindua mbio za Mwenge mwaka huu na ule utakaoandaa sherehe za kilele wafanye maandalizi mapema kwa kuzingatia utaratibu huo mpya utekelezwe ipoasavyo kwani tathimini yao italeta maana na manufaa iwapo yale mambo mazuri yatatekelezwa na wanaapobaini mapungufu na kero wachuke hatua ya kurekebisha kasoro na kero hizo ili zisijejitokeza katika shughuli hizo.
.