Copyright @ STAR TV LTD . All Rights Reserved.
Hayo yamebainishwa mjini Singida na mkurugenzi wa bima ya afya kanda ya kati bw Christopher Mapunda kwenye warsha juu ya utaratibu na uwanachama wa mfuko huo wa bima ya afya.
Amesema baada ya kufanyiwa marekebisho kwa sheria iliyounda mfuko huo mwaka huu, askari polisi, magereza, zimamoto na uhamiaji wanatarajiwa kuanza kuhudumiwa na bima hiyo kuanzia Julai mwaka huu.
Bw Mapunda amesema lengo ni kuunganisha nguvu baina ya watumishi na waajiri wao kwa kuchangia asilimia tatu ya mshahara kila mmoja kwa ajili ya kugharamiwa matibabu.
Baadhi ya washiriki wa warsha hiyo wamesema kuwa kuingizwa kwenye mpnago huo kutakuwa mkombozi kwao kutokana na kupanda kwa gharama za matibabu zilizokuwa zinawasumbua.
Mfuko wa taifa wa bima ya afya (NHIF) ulianzishwa mwaka 1999 kwa sheria namba 8 ukiwa na jukumu la kugharamia matibabu ya watumishi wa umma, wenzi wao na wategemezi wanne.
Bongo Beats every Monday to Saturday @ 1900hrs
Bonga na Startv every Monday to Saturday @ 1705hrs
Habari every Monday to Sunday @ 2000hrs