); bloginfo(

Category: Habari katika Picha

Sherehe za Mei Mosi Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk .Ali Mohamed Shein,akizungumza na wanayakazi wa Sekta mbali mbali za Serikali na Sekta Binafsi wakati wa Sherehe za Maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani (MEY DAY)zilizofanyika jana katika ukumbi wa Salama Bwawani Hotel Mjini Unguja,(kushoto) Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Zanzibar,Zahrani Mohamed Nassor,(kulia) Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee na Waziri wa Kazi,Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Haroun Ali Suleiman.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk .Ali Mohamed Shein,akimkabidhi   Fedha tasilim Margreth Peter Mathew wa Nelia Hotel & Resort Zanzibafr, Shilingi za Kitanzania Laki Saba,(700,000/=)  kupitia Chama cha wafanykazi (CHODAU) akiwa katika miongoni mwa wafanyakazi bora kwa mwaka 2012,wakati wa sherehe za siku ya wafanyakazi Duniani zilizofanyika katika ukumbi wa Salama Bwawani Hotel Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk .Ali Mohamed Shein,akimkabidhi   Fedha tasilim Kidawa Juma said Shilingi za Kitanzania Laki Mbili na Hamsini Elfu (250,000/=) Mfanyakazi Bora,wa Halmashauri  ya Wilaya ya Magharibi kupitia Chama cha wafanykazi (ZALGWU) akiwa katika miongoni mwa wafanyakazi bora kwa mwaka 2012,wakati wa sherehe za siku ya wafanyakazi Duniani zilizofanyika jana katika ukumbi wa Salama Hotel Bwawani. {Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.}
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati ) akishikana mikono na viongozi wakati wa Sherehe za  kilele cha Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani,na kuimba wimbo wa (Solidariti Foreva) wakinyanyua juu mikono kuonesha mshikamano katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja zilizofanyika sherehe hizo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati ) akishikana mikono na viongozi wakati wa Sherehe za  kilele cha Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani,na kuimba wimbo wa (Solidariti Foreva) wakinyanyua juu mikono kuonesha mshikamano katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja zilizofanyika sherehe hizo  jana.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0.0/10 (0 votes cast)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0 (from 0 votes)

JK aongoza Maadhimisho ya Mei Mosi kitaifa Tanga.

 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki kuimba wimbo wa wafanyakazi akiwa kashikana mikono na Rais wa Jumuiya ya Vyama vya wafanyakazi (TUCTA) Mh, Waziri wa Kazi na Ajira Mh Gaudence Kabaka (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh Galawa katika sherehe za Mei Mosi katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga Mei 1, 2012
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia katika sherehe za Mei Mosi katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga Mei 1, 2012
 Wafanyakazi wa Ofisi za Bunge wakiigiza kikao cha bunge wakati gari lao lilipokuwa linapita mbele ya Rais Dkt Jakaya Kikwete katika sherehe za Mei Mosi katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga Mei 1, 2012
 Wafanyakazi wakifuatilia maadghimisho hayo mkoani Tanga
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni tatu kama zawadi kwa  Mfanyakazi bora wa Tanesco Bi Anetha Chengula  katika sherehe za Mei Mosi katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga jana Mei 1, 2012
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0.0/10 (0 votes cast)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0 (from 0 votes)

Makamu wa Rais aweka jiwe la msingi BANC ABC.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi wakati alipokuwa akizindua rasmi jengo la BANC ABC jijini Arusha jana Aprili 16, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, na Mwenyekiti wa Bodi wa Benki ya ABC ya jijini Arusha, Dkt. Jonas Kipokola, wakifunua kitambaa kuashiria kuweka Jiwe la Msingi katika Benki hiyo mpya wakati Makamu alipofika jijini humo kuizindua rasmi  Aprili 16, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, na Mwenyekiti wa Bodi wa Benki ya ABC ya jijini Arusha, Dkt. Jonas Kipokola, wakifurahia baada ya kuzindua rasmi na kuweka Jiwe la Msingi katika Benki hiyo mpya wakati Makamu alipofika jijini humo kuizindua rasmi  Aprili 16, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa Benki ya ABC Tawi la Arusha, Anna Kavishe, kuhusu utendaji wa kazi na ramani ya jengo jipya la benki hiyo, baada ya kuizindua rasmi  Aprili 16, 2012, jijini Arusha. Wapili (kulia) ni Mke wa Makamu Mama Zakhia Bilal na Kulia kwa Makamu ni Mwenyekiti wa Bodi wa Benki hiyo, Jonas Kipokola.
Picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi huo. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0.0/10 (0 votes cast)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0 (from 0 votes)

Mwenyekiti wa Majeshi ya Polisi Afrika Mashariki atembelea Tanzania.

Mwenyekiti wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi Nchi za Mashariki mwa Africa ambaye pia ni Inspekta Jenerali wa Polisi Rwanda, Emmanuel Gasana (kulia) akizungumza na maofisa wakuu wa Jeshi la Polisi Tanzania leo jijini Dar es Salaam. IGP wa Rwanda yupo katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa kumi na tatu wa wakuu wa Majeshi ya Polisi wa EAPCCO, mkutano uliofanyika nchini Rwanda mwezi septemba 2011. Ziara hii ni pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya Majeshi ya nchi za mashariki mwa Afrika. Picha Na Hassan Mndeme wa Jeshi la Polisi.
Mwenyekiti wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi Nchi za Mashariki mwa Africa ambaye pia ni Inspekta Jenerali wa Polisi Rwanda, Emmanuel Gasana (kulia) akizungumza na maofisa wakuu wa Jeshi la Polisi Tanzania leo jijini Dar es Salaam. IGP wa Rwanda yupo katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa kumi na tatu wa wakuu wa Majeshi ya Polisi wa EAPCCO, mkutano uliofanyika nchini Rwanda mwezi septemba 2011. Ziara hii ni pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya Majeshi ya nchi za mashariki mwa Afrika. Picha Na Hassan Mndeme wa Jeshi la Polisi.
  

  Mwenyekiti wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi Nchi za Mashariki mwa Africa ambaye pia ni Inspekta Jenerali wa Polisi wa Rwanda, Emmanuel Gasana (kushoto) akiongozwa leo katika Makao makuu ya Jeshi la Polisi Tanzania na Kamishna wa Operesheni, Paul Chagonja aliopo nchini katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa kumi na tatu wa wakuu wa Majeshi ya Polisi wa EAPCCO, mkutano uliofanyika nchini Rwanda mwezi septemba 2011. Ziara hii ni pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya Majeshi ya nchi za mashariki mwa Afrika. Picha Na Hassan Mndeme wa Jeshi la Polisi.
 
Mwenyekiti wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi Nchi za Mashariki mwa Africa ambaye pia ni Inspekta Jenerali wa Polisi Rwanda, Emmanuel Gasana (kushoto) akisaini kitabu cha wageni katika ofisi za wizara ya Mambo ya Ndani leo jijini Dar es Salaam aliopo nchini katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa kumi na tatu wa wakuu wa Majeshi ya Polisi wa EAPCCO, mkutano uliofanyika nchini Rwanda mwezi septemba 2011. Ziara hii ni pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya Majeshi ya nchi za mashariki mwa Afrika. Kulia ni Kamishna wa Operesheni, Paul Chagonja  Picha Na Hassan Mndeme wa Jeshi la Polisi.
 
Mwenyekiti wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi Nchi za Mashariki mwa Africa ambaye pia ni Inspekta Jenerali wa Polisi Rwanda, Emmanuel Gasana (kushoto) akionyeshwa mazingira ya Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Tanzania na Kamishna wa Operesheni, Paul Chagonja leo jijini Dar es Salaam. IGP wa Rwanda yupo katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa kumi na tatu wa wakuu wa Majeshi ya Polisi wa EAPCCO, mkutano uliofanyika nchini Rwanda mwezi septemba 2011. Ziara hii ni pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya Majeshi ya nchi za mashariki mwa Afrika. Picha Na Hassan Mndeme wa Jeshi la Polisi.
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0.0/10 (0 votes cast)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0 (from 0 votes)

Ziara ya Rais Dk Shein kisiwani Pemba

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na wananchi waliojitokeza kumpokea katika uwanja wa karume Pemba alipowasili kisiwani humo kwa ziara maalum kuangalia maendeleo katika sekta mbali mbali za kijamii.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la MapinduziDk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Mtoto Suleiman Shaaban Juma,pamoja na wanachama wa Kampuni ya Mkipi  Miliki Tungamaa,kuzindua Mradi wa uzalishaji wa sabuni kwa kutumia mashine maalum ya Mkipi Miliki,jana akiwa katika ziara kisiwani Pemba,kuangalia maendeleo ya jamii.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la MapinduziDk.Ali Mohamed Shein,  akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mpango wa kuanzisha bednki ya Jamii ya Muwape Saccos Mtemani Wete Pemba, alipokuwa katika ziara ya kuangalia maendeleo katika sekta mbali mbali za Kijamii Mkoani humo,(kulia) Mize Khamis.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la MapinduziDk.Ali Mohamed Shein,akiangalia Sabuni iliyotengenezwa katika kampuni ya Mkipi Miliki Tungamaa,ambayo inayozalisha sabuni kwa kutumia mashine maalum,alipokuwa katika ziara ya kutembelea maendeleo katika Mkoa wa Kaskazini Pemba,(kulia) Mkurugenzi Mkuu  George M.Buchwafwe.
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0.0/10 (0 votes cast)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0 (from 0 votes)

Waziri Mkuu atembelea kiwanda cha A-Z Arusha.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua  utengenezaji  vyandarua na nguo katika kiwanda cha A to Z cha Arusha Aprili 15,2012. Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa kwanda hicho,  Anuj Shah. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua mbolea iliyorundikana kwenye maghala ya kiwanda cha mbolea cha Minjingu Mkoani Manyara wakati alipotembelea kiwanda hicho Aprili 16, 2012. Kiwanda hicho kimesimamisha uzalishaji baada ya mbolea yake kukosa soko. Kushoto  ni Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho, Tosky Hans. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na washiriki wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa wa Wakaguzi wa Hesabu za Serikali wa Nchi zinazoongea kiingereza barani Afrika kwenye hoteli ya Impala, Arusha Aprili 16, 2012. Kulia kwake ni  Mdhibiti na Mkaguzi  mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utouh. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na washiriki wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa wa Wakaguzi wa Hesabu za Serikali wa Nchi zinazoongea kiingereza barani Afrika kwenye hoteli ya Impala, Arusha Aprili 16, 2012. Kulia kwake ni  Mdhibiti na Mkaguzi  mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utouh. na kulia ni Naibu Waziri wa Fedha, Gregory Teu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0.0/10 (0 votes cast)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0 (from 0 votes)

Rais Kikwete akutana na Rais Mstaafu wa Brazil

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na na Rais Mstaafu wa Brazil Mh Luis Inancio Lula da Silva mara baada ya mazungumzo yao alipokwenda kumjulia hali jijini Sao Paulo April 16, 2012.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Rais Mstaafu wa Brazil Mh Luis Inancio Lula da Silva baada ya mazungumzo yao alipokwenda kumjulia hali jijini Sao Paulo April 16, 2012. 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na  Rais Mstaafu wa Brazil Mh Luis Inancio Lula da Silva alipokwenda kumjulia hali jijini Sao Paulo April 16, 2012. Kushoto ni balozi wa Tanzania nchini Brazil Mh Francis Malambugi na wa pili kushoto ni balozi wa Brazil nchini Tanzania Mh Francisco Carlos Luz.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Rais Mstaafu wa Brazil Mh Luis Inancio Lula da Silva alipokwenda kumjulia hali jijini Sao Paulo April 16, 2012.
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0.0/10 (0 votes cast)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0 (from 0 votes)

Makamu wa Rais aongoza waombolezaji kwenye kuaga mwili wa Marehemu Steven Kanumba

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Gharib Bilal akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu Steven Kanumba ulioagwa leo kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam huku viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini, Wanasiasa, Wanamuziki Waigizaji na watu maarufu wamejitokeza kuuaga mwili wa mwigizaji huo aliyekuwa maarufu zaidi nchini Tanzania na nje ya  nchi pia, Marehemu Steven Kanumba anazikwa mchana huu kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
Picha ya chini wa pili kutoka kushoto  ni Mama wa Marehemu Steven Kanumba Bi. Flora Mgoa akiwa katika hali ya majonzi mwisho kushoto ni Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka akimfariji Mama Kanumba
Mmoja wa waombolezaji akisidiwa na wafanyakazi wa msalaba mwekundu mara baada ya kuzimia katika msiba huo mkubwa.
Kutoka kulia ni Waziri wa Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo Dk. Emmanuel Nchimbi, Ridhiwan Kikwete, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni Idd Azzan na waombolezaji wengine wakiwa katika msiba huo.
Kundi maalum lililoandaliwa kwa nyimbo za maombolezo likiimba nyimbo za maombolezo katika katika msiba huo.
Jeneza la mwili wa marehemu Kanumba likiwa limewekwa tayari kwa waombolezaji kutoa heshima zao za mwisho
Ndugu  wa karibu wakielekea sehemu waliyotengewa kukaa.
Askari wa kike wakiweka sawa utaratibu wa waombolezaji kupita katika eneo hilo ili kukaa.
Rais wa Shirikisho la wasanii wa Filamu Saimon Mwakifwamba akizungumza katika msiba huo kutoa salamu zao za rambirambi kwa marehemu Steven Kanumba
Mmoja wa waombolezaji akipitishwa juu juu kwenye vichwa vya waombolezaji ili kupata huduma ya kwanza baada ya kuzirai, katikati anayetazama mbele ni Mussa Kisoky Mkurugenzi wa kampuni ya Sofia Production ya jijini Dar es salaam.
Mwigizaji Steven Jacob kushoto akizungumza  jambo na mbunge wa Maswa Mashariki Mh. John Shibuda katikati.
Mr Mtitu kulia akijadili jambo na mmoja wa waombolezaji wa
Utaratibu unapangwa na wanakamati wa kamati ya mazishi
Gari lililobeba mwili wa marehemu Kanumba linaondoka Leaders kwenda Makaburi ya Kinondoni huku likiwa limezungukwa na waombolezaji.
Umati wa waombolezaji ukiondoka kuelekea makaburi ya Kinondoni.
Jeneza lenye Mwili wa Marehemu,Steven Kanumba likiwasili kwenye Viwanja vya Leaders Club,jijini Dar es Salaam asubuhi hii.  Makamu wa Rais,Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Steven Kanumba asubuhi hii kwenye viwanja vya Leaders Club,Jijini Dar es Salaam.akifuatiwa na Mkewe,Pamoja na Mke wa Rais,Mama Salma Kikwete (mwenye nguo nyeupe kulia). Mh. Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu akitoa heshima za mwisho.
Kwaya maalum ikiimba nyimbo za maombolezao katika msimba huo kwenye viwanja vya Leaders
Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi akipiga sal;ute mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Steven Kanumba kama ishara ya kumkubali kwake na kutoa heshima kwa marehemu Steven Kanumba.
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0.0/10 (0 votes cast)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0 (from 0 votes)

WAZIRI MKUU NA MATUKIO BUNGENI DODOMA LEO .

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Viti Maalum, Zaynabu Vullu (kulia) na Mbunge wa Bariadi Mashariki John Cheyo kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Aprili 10, 2012.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa zamani wa Bariadi Magharibi,  Isaac Cheyo kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Aprili 10, 2012.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Newala na Waziri wa  Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawalaza Mikoa na Serikaliza Mitaa, Capt. Mstaafu George Mkuchika Katikati na Mbunge wa Viti Maalum, Pindi Chana (kulia)  kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Aprili 10, 2012.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu na Mbunge wa Ismani, William Lukuvi (kushoto) akizungumza na Mbunge wa Kibakwe, Gerge Simbachawene (kulia), Naibu Spika na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai (wapili kulia) na Mbunge wa Chilonwa, Hezekiah Chibulunje kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Aprili 10, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0.0/10 (0 votes cast)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0 (from 0 votes)

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA APOKEA KOMBE LA UEFA.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimkabidhi zawadi ya kinyago Mwakilishi mkazi wa shirika la Unoja wa mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), BW Oluseyi Bajulaye ambaye alikwenda ofisini kwa Wziri mkuu kuaga. Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akiwapungua watu waliofika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kushuhudia wakati alipokabidhiwa kombe la UEFA jijini Dar es salaam Machi 26, 2012.
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda kwa pamoja na Meneja Mkuu wa Bia ya Heinken Afrika Mashariki Bw.KoenMorshiu’s wakifunua kitambaa, kuonyesha kombe la Ulaya wakati Kampuni ya bia ya Heinken ambao ndiyo wadhamini wa kombe la Ulaya (UEFA) walipomkabidhi kombe hilo waziri mkuu ofisini kwake, Kampuni ya Henken pamoja na Shirikisho la mpira wa miguu la ulaya (UEFA) liko katika ziara ya kulitembeza kombe hilo katika nchi za Afrika na Amerika ya Kusini nchini Mexico na Asia nchini China na Tanzania na Kenya.
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda kwa pamoja na Meneja Mkuu wa Bia ya Heinken Afrika Mashariki Bw.KoenMorshiu’s wakipiga makofi mara baada ya kufunua kitambaa kuonyesha kombe la Ulaya UEFA.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akipiga picha na Kombe hilo pamoja na mawaziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, kulia ni Naibu Waziri wa wizara hiyo Dk Fenella Mukangara, wa pili kutoka kushoto ni Dk Emmanuel Nchini Waziri wa wizara hiyo na Makamu wa kwanza wa shirikisho la mpira miguu nchini Tanzania (TFF) Athuman Nyamlani. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0.0/10 (0 votes cast)
VN:F [1.9.22_1171]
Rating: 0 (from 0 votes)