‘Habari za Kimataifa’ Archives
Bunge la Ugiriki lapitisha mpango wa kubana matumizi.
Bunge la Ugiriki limepiga kura kuidhinisha mpango wa serikali wa kubana matumizi, na hivyo kufungua njia kwa mkopo mpya wa mabilioni ya euro kutoka Umoja wa Ulaya na wakopeshaji wengine. Baada ya mjadala mkali, mpango huo uliungwa mkono na wabunge 199 kati ya 278 waliopiga [Read More]
Wachina waliotekwa Sudan waachiliwa
Kundi la wafanyakazi kutoka China waliotekwa nyara nchini Sudan, wameachiliwa huru na kusafirishwa hadi Kenya, maafisa kutoka nchi hizo mbili wanasema. Wachina hao wanaofanya kazi za ujenzi waliachiliwa kwa kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu siku ya Jumanne, siku 11 [Read More]
Ajilipua katika kambi ya jeshi Nigeria.
Mtu mmoja aliyevaa nguo za kijeshi amejilipua nje ya kambi ya jeshi katika jiji la Kaduna nchini Nigeria, huku kukiwa na taarifa za mashambulio mengine, maafisa wanasema. Msemaji wa jeshi amesema wanajeshi walimpiga risasi lakini alifanikiwa kulilipua bomu katika gari [Read More]
Muswada “tata” warejea bungeni Uganda
Mbunge mmoja wa Uganda ameurejesha muswada wenye utata wa wapenzi wa jinsia moja, lakini kipengele cha hukumu ya kifo kimeondolewa, kwa kosa la vitendo kadhaa. Mwandishi wa BBC amesema wabunge walicheka, kupiga makofi na kushangilia wakisema “Muswada wetu, muswada [Read More]
Uhasama watokota kati ya Sudan Kusini na utawala wa Khartoum.
Uhasama kati ya serikali ya Sudan Kusini na utawala wa Khartoum kwa mara nyingine umechochewa na mzozo kuhusu mafuta yanayopatikana katika maeneo ya mipaka ya nchi hizo mbili. Wakimbizi wa Sudan Kusini Uchumi wa mataifa haya mawili unategemea sana mapato yanayotokana na [Read More]
Somalia kufukuza wananchi waliovamia majengo ya serikali.
Somalia imeanza shughuli kubwa ya kuwahamisha maelfu ya watu waliovamia na kuishi katika majengo ya serikali mjini Mogadishu. Meya wa Mogadishu ameiambia BBC kuwa watakaohamishwa hawatapewa nyumba za kuhamia kwa sababu wavamizi hao wamekuwa wakilipa kodi kwa wamiliki [Read More]
Kuendelea kwa machafuko, Urusi sasa kufanya majadiliana na Syria.
Msimamo wa Urusi kuhusu matukio nchini Syria umeghadhabisha sana baadhi ya serikali za kimagharibi. Waziri wa mashauri ya kigeni wa Marekani Hilary Clinton pamoja na chancellor wa ujerumani Angela Markel wameshutumu hatua ya Urusi na China ya kupiga kura ya turufu kupinga [Read More]
Ndege za Marekani zadaiwa kuuwa raia
Ripoti ya Shirika la waandishi wa habari wanaochunguza taarifa, lenye makao mjini London, inaonesha kuwa mamia ya raia wameuwawa katika mashambulio yaliyofanywa na ndege za Marekani zisokuwa na rubani kwenye maeneo ya Pakistan, katika miaka mitatu iliyopita. Ripoti hiyo, [Read More]
Utaliana yapata homa ya West Nile
Baridi ya juma hili Utaliana haikupata kuonekana kwa miaka 30. Na huku Wataliana wanatetemeka, wamepata habari nyengine zisokuwa za kawaida: kwamba wageni wamewasili katika kisiwa cha Sardinia, kutoka Afrika. Wingu la flamingo, au heroe, huvutia maelfu ya watu kila mwaka, [Read More]
Marekani kushinikiza rais Assad aondoke
Marekakani imesema kuwa mataifa ya kirafiki yanayoitakia Syria utawala wa Kidemokrasia yanapaswa kuungana katika kumshutumu kiongozi wa taifa hilo Rais Assad. Waziri wa mashauri ya Kigeni wa Marekani, Bi Hillary Clinton, alisema ni jambo la kusikitisha kuwa Urusi na Uchina [Read More]
